Kampuni Ya Kuuza Dawa Ya Green World

 

Kampuni Ya Green World Tanzania

Unatafuta Biashara Ya Mtaji Mdogo?

 

Leo napenda tuizungumzie kampuni ya kuuza dawa ya Geen World yenye ofisi zake mjini Dar Es Salaam. Katika ukurasa huu nitatoa maelezo kidogo kuhusu shughuli za kampuni hii, aina ya dawa ambazo huuzwa na kampuni hii na jinsi ambavyo wewe mtanzania unaweza kunufaika kwa kujiunga na kampuni hii ukafanya biashara na kupata maendeleo kwa mtaji mdogo sana. Nimeona ni lazima niizungumzie kampuni hii kwa sababu watanzania wengi tayari wamenufaika sana kupitia kampuni hii, wengi wao wanapata vipato vikubwa sana kwa mwezi na wengine wamefikia kupewa magari yenye thamani ya hadi shilingi milioni kumi na nane. Watu ninaowazungumzia si watu wenye elimu kubwa au waliokuwa na mitaji mikubwa sana, la hasha, ni watanzania wa kwaida tu waliokuwa na ari ya kufanya biashara na walipoisikia kampuni hii wakajiunga mara moja na kujituma ipasavyo.

Naomba ieleweke kwamba katika maelezo yangu nitatumia neno dawa ingawa maana halisi ya vitu ninavyoviongelea hapa ni virutubishi vya asili ambavyo vikitumiwa humsaidia  mtu kuiweka vizuri afya yake au aliyeathirika na magonjwa na kupona. Endelea kusoma ili uijue kampuni hii.

 

Ijue Kampuni Ya Green world

 

Green World USA ni kikundi cha makampuni ya kimataifa kinachoshughulika na utafiti wa kisayansi, uendelezaji na uzalishaji wa madawa ikiwa ni pamoja na dawa zinatozotokana na mimea na vipodozi kikiwa na makao yake makuu katika mji wa Michigan nchini Marekani na viwanda vyake vya uzalishaji huko South Carolina.

 

Prof Deming Li

 

 

Muasisi wa kampuni hii Dk. Deming Li alikuwa na dhamira moja kuu ya kutumia mimea na hasa mimea ya asili ya China na matokeo ya tafiti zake binafsi alizozifanya kupata hazina ya bidhaa zitakazomsaidia kila mtu popote pale alipo katika dunia yetu.

 

virutubisho vya Green World

 

 

Kampuni ya Green World iliundwa kutengeneza bidhaa zinazotokana na mimea na vitu vya asili kwa kutumia utaalamu wa hali ya juu wa kisasa. Kwa kushirikiana na vituo vya utafiti na vyuo vikuu mbalimbali, kikiwepo chuo kikuu cha Cornell (USA), kampuni hii imeweza kutengeneza bidhaa mbalimbali za tiba-lishe, bidhaa ambazo hadi sasa zimeleta na kutoa mchango mkubwa katika kuboresha afya ya binadamu. Dawa za kampuni hii zimepokelewa na zinatumika sana katika nchi za China, Marekani na nchi za kusini mashariki mwa bara la Asia hasa Indonesia.

 

Dawa Za Kampuni Ya Green World

 

Kampuni ya Green World USA hadi sasa imefanikiwa kutengeneza virutubisho vya asili vya aina tofauti (zaidi ya aina mia moja) ambavyo husambazwa katika nchi zaidi ya 50 duniani. Tunaweza kwa haraka haraka kuvigawanya virutubisho hivi au dawa hizi katika makundi kutokana na tatizo linalohusika. Green World wanazalisha virutubisho au dawa kwa ajili ya matatizo yafuatayo:

1.  Matatizo Ya Mifupa Na Viungio Vya Mifupa
2.  Matatizo Ya Maambukizi Ya wadudu
3.  Matatizo Ya Kuwa Na Uzito Mkubwa (Unene).
4.  Matatizo Ya Ubongo
5.  Magonjwa Ya Watoto
6.  Magonjwa Na Afya Ya Akina Mama
7.  Matatizo Na Afya Ya Mwanamme
8.  Afya Ya Macho
9.  Matatizo Ya Uyeyushaji Chakula Tumboni
10. Matatizo Ya Ngozi
11. Ukosefu Wa Kinga Ya Mwili
12. Matatizo Ya Moyo
13. Kansa

 

Jinsi Ya Kufanya Biashara Kwa Mtaji Mdogo Kabisa Na Kampuni Hii

 

Kufanya biashara na kampuni hii ni rahisi sana, unachotakiwa biashara kwa manesikukifanya ni kujiunga kwa TZS 30,000/ tu. Ukishajiunga kwa kiasi hicho cha pesa utapewa kitambulisho cha kampuni na kifurushi cha kuanzia chenye maelezo muhimu na utatakiwa kuhudhuria mafunzo ya bure ya jinsi ya kuendesha biashara hii. Baada ya hapo utatakiwa kutafuta wagonjwa na kuwauzia dawa kutoka kampuni hii. Utauziwa dawa kwa bei ya jumla kama msambazaji wa kampuni na kuziuza kwa faida utakayoiweka mfukoni mwako. Kusudi uweze kupata kipato kikubwa zaidi, utawajibika kuwashawishi ndugu na rafiki wengine kujiunga na biashara hii, hapo ndipo utakapojenga timu yako. Malipo utakayopata kwa mwezi yatalingana na ukubwa wa timu uliyoijenga chini yako. Rahisi kabisa!

Biashara hii  hufanywa kwa njia ya mawasiliano ya mdomo (word of mouth) hivyo inamfaa mtu yeyote, ni biashara kwa kwa akina mama wa nyumbani, ni biashara kwa mwanafunzi chuoni, ni biashara kwa mfanyakazi katika ofisi, biashara kwa mwalimu wa shule, biashara bora kwa nesi katika hospitali…  ni biashara ya mtaji mdogo kwa mtu yeyote! Ili kuona kwa nini biashara hii ni bora kwa jamii ya watu wetu wa Tanzania, soma ukurasa wa “Ubora Wa Kampuni Ya Green world Tanzania“.

Wapo walionufaika na wanaolipwa pesa nyingi kwa mwezi katika kila kundi nililolitaja hapo juu. Usisite kwamba utashindwa kujenga timu yako kwa sababu utapewa mafunzo na msaada kutoka kwa mtu aliyekushauri kujiunga na biashara hii na utaweza tu.

 

wanachama wa kampuni ya green world tanzania

 

Pichani hapo juu ni baadhi ya watanzania waliofanya vizuri katika biashara hii wakipewa tuzo mbalimbali ikiwa ni pamoja na magari na fursa ya kutembelea nchi ya China kwa gharama ya kampuni.

 

Kujua jinsi ya kununua bidhaa za kampuni hii kwa matumizi binafsi, rejea ukurasa wetu wa “Jiunge na Green World, kuboresha afya yako.”

 

 

Kwa mawasiliano tuma ujumbe wako kupitia ukurasa huu kwa kujaza fomu hapa chini , au tuma barua pepe kwa anuani promota927@gmail.com au piga simu kwenye nambari zifuatazo: 0655 858027 au 0756 181651.

 

Pata maelezo ya kampuni ya TREVO TANZANIA ambayo inasambaza kirutubisho cha Trevo kwa kusoma ukurasa wa “Kampuni Ya Kirutubisho Cha Trevo”. Ni kampuni nyingine ambayo inawaruhusu watanzania kufanya biashara ya mtandao na kujipatia faida kubwa.

 

Tafadhali tembelea blog yetu kujisomea mada mbali mbali zinazohusu biashara za mtandao na fursa za kufanya biashara za mtandao zinazotolewa na kampuni za Green World Tanzania na Trevo Tanzania Ltd. Humo unaweza kuona wasomaji wengine wana maoni gani kuhusu mada zetu tunazoziandika. Pia unakaribishwa kuona video mbali mabali zinazohusu biashara ya mtandao ya kampuni ya Green World kwenye channel yetu ya YouTube.

 

 

Kutembelea blog bofya HAPA.
Kutembelea channel yetu ya YouTube bofya HAPA.

 

Jina Lako

Anuani Ya Barua Pepe

Namba Yako Ya Simu

Kichwa Cha Habari

Swali Au Maoni Yako

Pata Mahitaji Yako Ya Dawa Za Nje Kwa Matatizo Yanayokusumbua Ukiwa Tanzania. Boresha Afya Yako Kupitia Tovuti Hii