Tujue SagalaWebs

 

SagalaWebs, Ni Nani Hawa?

 

Sagalawebs ni kampuni inayojumlisha kikundi cha watanzania ambao kwa muda mrefu wamekuwa wakijihusisha na biashara za kwenye mitandao. Biashara hizo ni pamoja na Affiliate Marketing, Internet marketing na Network marketing. Katika kufanya biashara hizo, wamejifunza mambo mengi kutoka makampuni ya wenzetu wa nje kuhusu biashara za kisasa za kwenye mitandao.

 

karibu green world tanzania

Pichani hapo juu ni ndugu Laurian Mwajombe, mmiliki na webmaster wa tovuti za sagalawebs.com. Unaweza kuungana naye kwenye kurasa za Google+ hapa.

Moja ya mfano mzuri wa mambo ambayo Sagalawebs imekuwa ikifanya nje ya nchi ni tovuti mama www.sagalawebs.com ambayo inatoa mafunzo mbalimbali kuhusu ufanyaji wa biashara ukiwa nyumbani kwa kutumia mtandao na ujenzi wa tovuti za kisasa. Watu mbalimbali kutoka pande zote za dunia huingia katika tovuti hii na kunufaika nayo. Kwa sasa ( August 2014 ), tovuti hii ina wastani wa wasomaji 500-1000 kwa siku na ina umri wa miezi 7 tu.

 

 Madhumuni Ya Tovuti Hii

 

Baada ya kuona mafanikio ya nje, tukajiuliza: Kwa nini tusilete ujuzi huu nyumbani? Hii ndio sababu ya kuanzisha tovuti nyingine mbili zote zikilenga mambo ya hapa nyumbani.

 

Tovuti ya kwanza ni www.localmarketing.sagalawebs.com ambayo inalenga kujenga tovuti za kisasa na kuwaelimisha wafanya bishara mbalimbali kuhusu mbinu za kisasa za kufanya biashara za kwenye mitandao. Hapa tunagusia mobile marketing, local business listings, na social media marketing. Yote haya yanaelezwa vizuri katika tovuti hii.

 

Tovuti ya pili ni hii ambayo lengo kuu ni kukusanya products ambazo watu wanazitumia sehemu mbalimbali za dunia, kuziorodhesha na kuzitolea tafsiri kwa kiswahili  ili hata mwananchi wa kawaida aweze kuzielewa products hizo, na endapo atapenda kuzitumia, tutamsaidia kuziagiza.

Ili watu waweze kufikia kuziona products hizo, tulianza kwanza kwa kuelezea magonjwa au matatizo mbalimbali ya kiafya  tukiwa na imani kuwa mtu ataingia kwenye mtandao kutafuta ufumbuzi wa tatizo lake na si products, na ndipo atakapopata taarifa ya products ambazo zinaweza kumwondolea tatizo lake, na si kinyume.

Katika tovuti hii pia tumejaribu kuelezea machache kuhusu biashara za mtandao, hii ni kwa sababu kuna watanzania na watu wa nchi za jirani wengi sana ambao kwa muda mrefu sasa wamekuwa wakijihusisha na biashara hizo na hasa za kuuza products za makampuni ya kutoka nje. Hivyo basi, tuliona ingefaa angalau kwa kifupi tuelezee nini maana ya biashara za mtandao, faida na hasara zake na vitu vya kuzingatia ili waweze kuzifanya biashara hizi kwa ufanisi.

Tumechagua baadhi ya kampuni tulizoziona kuwa zimeandaliwa kwa misingi mizuri na ambazo zimekuwa zikiwanufaisha watanzania katika kubadili maisha yao na kuzielezea ili wale ambao wanahitaji kuanza kufanya biashara za mtandao waanze vizuri na si kuangukia kwenye mikono ya kampuni mbovu. Hapa tumezigusia kampuni za Green World (Tanzania) na Trevo Tanzania Limited.

Si hayo tu, endapo utapenda kujua zaidi wasiliana nasi.

Kwa maelezo zaidi na ya kina, tuma ujumbe kupitia ukurasa huu hapa chini kwa kujaza fomu, au tutumie barua pepe kupitia mwajombelau14@gmail.com au tupigie simu kwa namba zifuatazo: +255 655 858027 au +255 756 181651.

Tafadhali ungana nasi kwenye ukurasa wa facebook wa LINDA AFYA YAKO ili upate mfululizo wa mada zetu zinazohusu afya ya binadamu na jinsi ya kuanza na kufanya biashara za mtandao zinazohusu virutubisho vya mwili kwa mtaji mdogo kabisa. Tunaomba uweke LIKE kwenye ukurasa huo endapo utakuwa umependezewa na mada zetu.

 

Jina Lako

Anuani Ya Barua Pepe

Kichwa Cha Habari

Swali Au Maoni

 

Pata Mahitaji Yako Ya Dawa Za Nje Kwa Matatizo Yanayokusumbua Ukiwa Tanzania. Boresha Afya Yako Kupitia Tovuti Hii