SEMINA KUHUSU ELIMU YA AFYA YA MWANAMKE

 

 

semia za green world ndogo

 

 

Kufuatia mahitaji ya jamii kuhusu elimu ya afya, kampuni ya Green World imaeanza kuendesha semina katika ofisi yake ya Dar
Es Salaam ili kuitoa elimu hiyo kwa wananchi. Elimu hii inatolewa BURE kabisa kila siku ya jumamosi kuanzia saa 4.00 asubuhi hadi saa 6.00 mchana.

Jumamosi ya tarehe 8 Aprili 2017, daktari Frank alitoa elimu kuhusu afya ya saratani ya maziwa na shingo ya uzazi. Daktari alieleza kwa kutumia lugha nyepesi chanzo cha saratani hizi, namna ya kujikinga, dalili zake na tiba ambazo hutolewa pale ambapo imebainika kuwa una tatizo.

 
Baada ya maelezo ya Dokta Frank, ndugu Mwajombe, mwanachama wa kampuni hiyo ya Green World alielezea kuhusu bidhaa zitokanazo na mimea zinazotengenezwa na kampuni hiyo zinavyoweza kuzuia saratani hizi au kusaidia uponyaji wake.

 

 

picha ya laurian

 

 

 

Baada ya kipindi cha maswali na majibu, wananchi wenye matatizo walipewa fursa ya kumwona daktari huyo na kumweleza matatizo waliyokuwa nayo, ambapo walijibiwa na kupewa ushauri Bure Kabisa!

Kampuni itaendelea na mafunzo haya jumamosi ijayo ambapo wananchi wanakaribishwa kuja kwa wingi kupata mafunzo haya yanayotolewa bure kabisa.

 

Laurian.

Semina Ya Green World Kibaya- Kiteto

 

Kiteto Green World Group picture

 

Katika mfulululizo wa mafunzo kwa wageni yanayotolewa na kampuni ya Green World, mwezi March 2017, tarehe 5, semina ilifanyika katika mji wa Kibaya- Kiteto. Semina hiyo iliandaliwa na mwanachama Thomas Mpalazi wa mji huo na mwanachama mmoja, ndugu Laurian Mwajombe, alitoka Dar Es Salaam kwenda Kiteto kushirikiana naye kutoa mafunzo hayo.

Mafunzo yalianza saa 10.30 na yalifanyika katika ukumbi wa Community uliopo hapo mjini Kiteto.

Wageni kwa ujumla walionyesha hamasa ya juu ya kuijua fursa hii na walikuwa makini sana katika kusikiliza yale yaliyofundishwa. Kuonyesha kuwa walifuatilia vizuri kile kilichofundishwa, waliuliza maswali mengi na ya msingi mara baada ya kupewa nafasi ya kuuliza maswali yao.

 

semina ya Green world Kibaya-Kiteto

 

Wengi wa waliohudhuria semina hiyo, waliomba kupewa nafasi nyingine kama hii ili waweze kuwajulisha ndugu zao ambao hawakupata bahati ya kuhudhuria semina hii ya mwanzao.

 

Laurian.

Semina Ya Green World – Nzega – Desemba 2016

 

John Bwana  semina ya Nzega

 

Kutokana na kuwa watu wengi wa mjini Mwanza wameona ubora wa bidhaa za kampuni ya Green World na kuifurahia fursa ya biashara inayotolewa na kampuni hiyo, ombi la kufanya semina mjini Nzega ili ndugu zao waweze pia kunafaika lilitolewa. Mkufunzi wa kampuni ndugu Victor, aliongozana na wanachama wawili wa kampuni kutoka Dar Es Salaam, ndugu Hilda Mahende na ndugu Laurian Mwajombe, ili kufanya semina katika mji huo wa Nzega. Pamoja nao, wanachama wawili kutoka Mwanza, ndugu John Bwana na ndugu Charles Ngalula walijumuika kwenye semina hiyo.

Semina ilifanyika katika ukumbi wa Ukwala Lodge siku ya jumamosi ya tarehe 17 Desemba 2016. Mwanachama mwenyeji wa mji huo, ndugu Zuhura Salum ndiye aliyefungua semina hiyo mnamo saa 10 ya alasiri.

Baada ya ufunguzi, ndugu John Bwana kutoka Mwanza alitoa mafunzo kuhusu historia ya kampuni ya Green World, bidhaa zinazosambazwa na kampuni hiyo na umuhimu wa kutumia bidhaa za virutubishi katika ulimwengu wa sasa uliondelea kisayansi na kiteknolojia.

Katika sehemu ya pili, mkufunzi kutoka Dar, ndugu Victor, alitoa mafunzo ya jinsi mwanachama anavyoweza kunufaika kimapato na kubadili kabisa maisha yake katika kipindi kifupi tu.

 

semina ya nzega

 

Tofauti na miji mingine mingi, watu wa Nzega walijitokeza kwa wingi na kuonyesha umakini wa hali ya juu sana katika kusikiliza yale yaliyofundishwa na kudhihirisha hilo, waliuliza maswali mengi na ya msingi sana.

Mwisho kabisa, muda ulitolewa kwa wale waliopendezewa na fursa hiyo ya biashara ili waweze kujiunga, ambapo baadhi wajiunga moja kwa moja.

 

 

Mkutano Wa Green World – Gold Crest Hotel Mwanza – 26 Novemba 2016.

 

Mkutano wa Green World, Gold Crest Hotel, 26 Novemba 2016

 

Kampuni ya Green World hutoa kila aina ya nyezo na mafunzo ili kumwezesha mwanachama wake kufanya kazi zake kwa urahisi na ufanisi zaidi. Mwezi Septemba 2016, kulikuwa na mfululizo wa semina zilizofanywa na mkufunzi mkuu wa kampuni hiyo, ndugu Budiman kutoka Canada, ambaye alitembelea miji ya Morogoro, Mbeya, Arusha, Dodoma na Mwanza.

Kuanzia 24 hadi 26 Novemba 2016, wanachama wawili kutoka ofisi ya Dar Es Salaam, ndugu Hilda Mahende na ndugu Laurian Mwajombe, waliendesha mafunzo katika jiji la Mwanza wakiandamana na mkufunzi wa kampuni ndugu Victor.

Tarehe 24 Novemba 2016, mafunzo yalifanyika katika hoteli ya Vizano kuanzia saa 9 alasiri, ambapo wanachama wapya walifunzwa (New Distributor Training). Siku iliyofuata, wanachama walipewa mafunzo katika hoteli hiyo hiyo yaliyolenga kuwapa mbinu za kuzianza biashara zao kwa ufanisi zaidi (Star Training).

 

Mkutano wa Gold Crest Hotel, Mwanza

Video Ya mkutano wa Green World uliofanyika Gold Crest Hotel Mwanza.

 

Mafunzo katika mji huo wa kanda ya ziwa yalihitimishwa siku ya jumamosi, tarehe 26 Novemba 2016, ambapo watu wote walikaribishwa katika ukumbi wa Mandela wa hoteli ya Gold Crest, na maelezo ya kina ya fursa ya biashara ya kampuni ya Green World yalitolewa.

Kwa ujumla, mafunzo hayo yalikuwa na mafanikio makubwa na wananchi wa mji huo walifurahishwa sana na fursa hii. Wananchi walijitokeza toka miji ya karibu ya Geita, Kwimba, Nzega, Musoma na hata Tabora. Wengi walijiunga ili waanze kubadili maisha yao kupitia fursa hii iliyo tofauti na nyingi ambazo zinatolewa hapa nchini.

Baadhi ya wananchi kutoka kampuni nyingine zinazotoa fursa za biashara walikiri kuwa hii ilikuwa fursa ya kipekee kutokana na kuwa ilikuwa na mpango rahisi wa kukua kibiashara tofauti na kampuni nyingi ambazo hutaka mwanachama kuanza kutetea upya daraja lake kila mwezi na kutoa malipo kutokana na idadi fulani tu ya vizazi vilivyo chini yao.

 

Mkutano wa Gold Crest Hotel Mwanza

 

Kikubwa zaidi ni shuhuda halisi kuhusu utendaji kazi wa bidhaa za kampuni hii na bei za bidhaa ambazo hata mwananchi wa kawaida anaweza kuzimudu, bila kusahau uhakika wa kupata bidhaa wakiwa hapo hapo mjini Mwanza na malipo yao kila mwisho wa Mwezi.

Laurian.

Mkutano Wa Fursa Ya Biashara Ya Kampuni Ya Green World – MWANZA

 

Mkutano Wa Fursa Ya Biashara Ya Kampuni Ya Green World – MWANZA

 

Gold Crest Hotel mwanza

 

Jiulize maswali yafuatayo:

 

1. Jee, ninapenda kupata kipato cha ziada?
2. Ninapenda fursa ya kufanya biashara binafsi?
3. Ninapenda kujiajiri?
4. Nina ndoto za kumiliki gari nzuri au kuwa na nyumba nzuri au kusafiri nje?
5. Ninapenda uhuru wa muda na wa kipesa?

Kama umejibu NDIYO kwa maswali angalau matatu katika hayo, usikose kuitumia nafasi hii:

Kampuni ya Green World Tanzania itafanya mkutano mkubwa katika hoteli ya Gold Crest, iliyoko mjini Mwanza, siku ya jumamosi ya tarehe 26, Novemba 2016.

Mamia ya wakazi wa Mwaza wanategemewa kuhudhuria mkutano huu kutokana na kuwa mji huo una wanachama wengi ambao tayari wamesambaza huduma za kampuni hii na wananchi wengi kuona kuwa bidhaa za kampuni hii zinatoa matokeo mazuri sana katika kuboresha afya zao. Wengi wamaeondokewa na matatizo yaliyowasumbuakwa muda mrefu.

Mbali na kuondoa matatizo ya kiafya, wanachama hao wamejihakikishia wenyewe kuwa kampuni inatoa malipo mazuri kila mwezi kwa kazi waifanyayo.

Historia ya kukua kwa kampuni hii mjini Mwanza inaanzia Desemba 2015 ambapo kwa mara ya kwanza kampuni ilifanya mkutano wake katika hoteli ya New Mwanza Hotel, na kufuatiwa na mkutano mwingine uliofanyika April 2016 katika hoteli hiyo hiyo.

 

green world group photo mwanza

 

Septemba 2106 ndipo mkufunzi wa kampuni ya Green World kutoka Canada, ndugu Budiman alipowasili na kufanya mkutano mkubwa katika hoteli ya Gold Crest. Kipindi chote hiki wananchi wamakuwa wakijihakikishia ukweli wa mafunzo yanayotolewa na kampuni.

Ni fursa kwako wewe ambaye umekuwa ukihangaika kutafuta kitu cha kweli cha kukuwezesha kutimiza ndoto zako.

Mkutano huu utatanguliwa na siku 2 za mafunzo kwa wanachama wa zamani katika hoteli ya Vizano. Ratiba nzima ni kama ifuatavyo:

 

 

 

Tarehe 24 Novemba 2016  – Vizano Hotel – Wanachama wa zamani
Tarehe 25 Novemba 2016  – Vizano Hotel  – Wanachama wa zamani
Tarehe 26 Novemba 2016  – Gold Crest Hotel –  Watu Wote

 
Kiingilio ni BURE kabisa!

 

Kupata maelezo ya kampuni ya Green World bofya HAPA.

Semina Ya Budiman Palace Hotel – Arusha

 

Semina ya Budiman Arusha

 

Katika mfululizo wa semina za mkufunzi kutoka Toronto Canada, ndugu Budiman, ya mwisho ilifanyika siku ya jumamosi ya tarehe 1 Oktoba 2016. Semina hii ilifanyika mjini Arusha katika ukumbi wa Jumbo Hall na ilianza muda wa saa 10 jioni.

Kama ilivyotarajiwa, wakazi wa mji wa Arusha walikuja kwa wingi kumsikiliza mkufunzi huyu wa kimataifa. Semina hii ilianza kwa mkufunzi kuitambulisha kampuni ya Green World International. Alitoa historia ya kampuni hii na kutoa mifano ya watu wengi walioweza kunufaika na kampuni ya Green World katika kuboresha afya zao za kimwili na afya za mifuko yao.

Kivutio kikubwa katika semina hii ni maelezo yaliyotolewa na mwanachama wa kampuni hii ya Green World, ndugu Mbuya, ambaye ni mwenyeji wa Arusha alipoelezea mafanikio yake. Mwanachama huyo alieleza kuwa alijiunga na kampuni hii mwaka 2008 na hadi sasa pamoja na kuwa amekuwa akipata kipato kikubwa kila mwezi, ameweza kupata ziara zaidi ya sita za kwenda kupumzika nje ya nchi na zawadi za magari 15 kila moja likiwa na thamani ya Tshs. milioni 20.

Semina hii ilifungwa kwa namna ya kipekee pale sista wa madhehebu ya kikatoliki alipotoa sala iliyoambatana na wimbo mtamu aliouimba kwa lugha ya kiingereza. Kwa hakika waliohudhuria semina hii walipata mafunzo yenye thamani kubwa, kiingilio kikiwa ni BURE – kwa hisani ya mkufunzi huyo.

Mkufunzi huyo anatarajiwa kuondoka tarehe 6 Oktoba, kuelekea kwao Canada.

 

Laurian.

Semina Ya Budiman Mwanza – 17 Septemba 2016

 

Semina Mwanza 17 sep 2016

 

Katika mfululizo wa semina zinazofanywa na mkufunzi kutoka Toronto Canada, ndugu Budiman, moja na mabayo ilikuwa na mwamko mkubwa sana hadi sasa ni ile ambayo ilifanyika katika mji wa Mwanza katika ukumbi wa Mandela ndani ya hoteli ya Gold Crest. Semina hiyo iliyoanza saa 9 alasiri ilihudhuriwa na wanachama na wageni walioalikwa wapatao 200 na kuufanya ukumbi huo kufurika kabisa.

Katika semina hiyo, ndugu Budiman aliielezea kampuni ya Green World akianza na historia yake, mafanikio yake na mwitikio wa watu duniani kuhusu kampuni hii. Aliezea kwa ufasaha kuhusu umuhimu wa kutumia virutubishi vya kiada katika karne hii ya maendeleo makubwa ya sayansi na teknolojia tunayoishi na kwa nini virutubishi vya Green World ndivyo bora katiak kukidhi haja hiyo. Pia alielezea jinsi mtu mwenye ari ya kuona anabadilika katika maisha yake kiafya na kiuchumi anavyoweza kunufaika na kampuni hii.

Siku iliyofuata, tarehe 18 septemba 2016, katika ukumbi huo huo, ndugu Budiman aliendelea na semina na kutoa mafunzo ya awali ya jinsi ya kuanza biashara na kampuni hii ya Green World. Alieleza kwa nini kuwa na NDOTO ndicho kitu cha kwanza katika kuianza biashara hii. Pia alisisitiza umuhimu wa kuwa na malengo na akafundisha namna ya kuandika malengo. Akitoa mifano iliyowafurahisha wengi, aliweza kuwatia hamasa hata wale ambao walikuwa hawajajiunga na kampuni hii kujiunga mara moja. Alielezea jinsi yeye binafsi alivyokuwa na ndoto ya kuendesha gari ya kifahari aina ya BMW na kwenda kwenye yard ya magari na kuulizia kuhusu gari hilo alilolipenda – wakati huo akiwa hana pesa, na karudi nyumbani kwake na kuanza kufanya kazi kwa nguvu akiwa na wazo moja tu kichwani, la kupata gari la aina ya BMW aliloliulizia kwenye ile yard. Baada ya mwaka mmoja alipewa gari alilotaka BURE na kampuni ya Green World.

Semina hizi zinaendelea hadi tarehe 6 Oktoba siku ambayo ndugu Budiman ataondoka na kurudi kwake Canada.

 

Mafunzo ya Mwanza

VIDEO YA MAFUNZO YA BUDIMAN _ MWANZA

 

Wakazi na wanachama wa Arusha mnakumbushwa kuwa nafasi hii adimu ya kumsikiliza mkufunzi huyu wa kimataifa mtaipata siku ya tarehe 1 Oktoba 2016. Hakuna kiingilio kwenye semina hizi na hakuna ubaguzi wa kipato au elimu – NI KWA WOTE!

 

Laurian

KAMPUNI YA GREEN WORLD YAANZA SEMINA ZA MWEZI MMOJA

 

Semina ya Budiman iliyoanza 7 septemba 2016

 

Pamoja na kuwa kampuni ya Green World inatoa nyezo nyingi za aina tofauti ili kuwawezesha wanachama wake kufanya kazi kwa ufanisi, haijasahau kuhakikisha kuwa mafunzo ya kina yanatolewa kwa wanachama wake. Kuna mafunzo yanayotolewa mara kwa mara katika ofisi za kampuni hiyo, na mara chache, analetwa mkufunzi wa nje ili wanachama wake wapate uzoefu wa nchi nyingine katika kuifanya biashara ya kampuni hiyo.

Kuanzia leo tarehe 7 Septemba 2016, mkufunzi mkuu wa kampuni mwenye makao yake makuu kwenye mji wa Ontario Canada, ndugu Budiman, ameanza mafunzo katika ofisi ya kampuni hiyo iliyoko eneo la Upanga, makabala na makao makuu ya JWTZ. Mafunzo haya yatafululiza kwa kipindi cha takribani mwezi mmoja. Mafunzo

 

Screenshot_1

 

yatatolewa kwa wanachama wapya, na kuna mafunzo ya viongozi – wale ambao tayari wamekuwepo ndani ya kampuni hiyo kwa kipindi kirefu na waliofikia ngazi za juu. Lengo ni kuhakikisha kuwa wanachama wote wanaijua vizuri biashara ya kampuni hiyo na kuwawezesha kuifanya kwa ufanisi zaidi.

Mafunzo yataendelea katika ofisi ya kampuni hii kila siku nne za kwanza za wiki, yaani, jumatatu hadi alhamisi.

Katika kuhakikisha kuwa wanachama walio nje ya Dar Es Salaam nao wanapata mafunzo hayo, mkufunzi huyu ataelekea katika miji ya Dodoma, Mwanza, Mbeya na Arusha. Ratiba ya nje ya Dar Es Salaam kwa sasa hivi ni kama ifuatavyo:

 

Dodoma – 10/9/2016
Mwanza – 17/9/2016 – Gold Crest Hotel
Mbeya  – 24/9/2016
Arusha – 1/10/2016

 

 

Kama wewe ni mtu unayependa kuona kuwa umetimiza ndoto zako za kufikia maisha ya uhuru, usikose kuhudhuria semina hizi za mmoja wa wakufunzi wanaoheshimika katika dunia hii. Gharama za kuhudhuria semina hizi ambazo zina thamani ya dola nyingi ni BURE – kwa hisani ya ndugu Budiman.

Wanachama hai wa kampuni ya Green World wanakumbushwa kuwa hakuna nafasi ya kuilinganisha na hii katika kujenga jumuia zao za wafanya biashara wa Green World. Wanaombwa kuhakikisha kuwa wanawapa taarifa watu wengi kadri watakavyoweza.

 

Laurian.

Wanachama Sita Wa Green World Ziarani China

 

watanzania ziarani china 2016 mei 19

 

 

Kampuni ya Green World ina viwanda vyake viwili vya kutengeneza bidhaa zinazotokana na mimiea huko nchini China. Viwanda hivyo viwili vipo katika miji ya Nanjing na Tianjin. Viwanda katika miji hiyo hutengeneza bidhaa baada ya matokeo ya utafiti unaofanyika katika vyuo vikuu vya huko Marekani. Moja ya vyuo vikuu hivyo ambavyo ni vituo vya utafiti ni Cornell University ambako muasisi wa kampuni hii, Dr Deming Li, alihitimu masomo yake katika fani ya microbiology na kupata shahada ya uzamifu.

Katika siku za karibuni, kampuni ya Green World imeanza kutengeneza bidhaa zinazotokana na mmea wa strawberry katika kiwanda chake cha mjini Nanjing. Pia kampuni imeanza kutengeneza mbolea itokanayo na viumbe hai, Green World Nutriplant Organic Fertilizer, katika kiwanda chake cha mji huo.

 

hilda wa green world ziarani china

 

Baada ya ufanisi mkubwa wa bidhaa za strawberry, kampuni imeandaa tamasha kusherehekea mafanikio hayo.

Kufanikisha na kuwanufaisha pia wanachama wa kampuni hiyo walio nje ya China, kampuni imawalika wanachama wake kutoka nchi mbalimbali ulimwenguni kuhudhuria tamasha hilo. Wanachama hao watapewa pia fursa ya kutembelea mji wa Shanghai, sehemu za kununua bidhaa za kibiashara na za utalii za mji wa Nanjing.

 

ziara ya china

Wana-Green World Wakiwa Kwenye Uwanja Wa Ndege DSM Kabla Ya Kuondoka Mei 19 2019

 

Nchi ya Tanzania imepewa mwaliko huo na wanachama 6 waliondoka nchini tarehe 19 Mei 2016 kuungana na wenzao wa mataifa mbalimbali. Wanachama wa Green world walioondoka siku hiyo walikuwa ni Scholastica Gwayde, Cecilia Mosha, Martha Tluway, Geofrey Alal, Hilda Mahende, Hanisha Semfuko na Dr. Highness Kaira.

 

wana-green world china mei 19 2016
Baada ya kutembelea sehemu za biashara, kiutalii na kuhudhuria tamasha hilo, wanachama hao wanategemewa kurudi nchini tarehe 27 mei 2016.

 

ziara ya watanzania china mei 19 2016

 
Usisite kutoa maoni au kuuliza maswali uliyo nayo kuhusu mada hii. Tutafurahi kuona kuwa tumekujibu kwa wakati na kwa ufasaha.

 

Tafadhali ungana nasi kwenye ukurasa wa facebook wa LINDA AFYA YAKO ili upate mfululizo wa mada zetu zinazohusu afya ya binadamu na jinsi ya kuanza na kufanya biashara za mtandao zinazohusu virutubisho vya mwili kwa mtaji mdogo kabisa. Tunaomba uweke LIKE kwenye ukurasa huo endapo utakuwa umependezewa na mada zetu.

 
Laurian.

Semina Ya Matumizi Ya Mbolea (Organic Fertilizer) – Green World Tanzania

mafunzo ya mbolea

Hisilicon K3

Kuna aina nyingi za mbolea ambazo wakulima wanazitumia ili kuyafanya mazao yao kukua kwa haraka na kutoa mazao mengi. Zama za kale watu walitumia mbolea ambazo walizitengeneza wenyewe. Kwenye miaka ya 60 na 70, nakumbuka wanafunzi walikuwa na somo la namna ya kutegeneza BIWI. Hili lilikuwa ni shimo lililochimbwa na baadaye majani na kinyesi cha wanyama kufukiwa ndani ya shimo hilo kwa muda fulani. Baada ya mda huo, shimo hili lilifukuliwa na mkulima alikuwa amepata mbolea nzuri kwa ajili bustani na mashamba yake.

Baadaye zilikuja mbolea ambazo ziliagizwa kutoka nje ya nchi au kutengenezwa na viwanda vyetu wenyewe. Mbolea za viwanda vya Tanga na Minjngu (Arusha) ni mifano ya mbolea hizi.

Wataalamu wa miaka ya sasa wanatufundisha kuwa mbolea hizi za viwandani (Inorganic Fertizers) zina madhara mengi na wamekuja na aina mpya ya mbolea ambazo wanaziita Organic Fertilizers.

Kampuni ya Green World ambayo ina vituo vyake vya utafiti nchini Marekani na viwanda vyake katika miji ya Tianjin na Nanjing huko China, inatengeneza mbolea iitwayo Nutriplant Organic Plus Fertilizer (NOPF). Mbolea hii ni ya majimaji na hutunzwa ndani ya kichupa cha plastiki chenye ujazo wa lita moja.

 

Mbolea -  green world

 

Katika semina iliyofanywa katika ukumbi wa kampuni hiyo ulio ndani ya ofisi za kampuni hiyo huko Upanga, Dar es Salaam, wataalamu wawili kutoka China walielezea manufaa ya mbolea hiyo kwa kutoa matokeo ya tafiti walizozifanya katika mashamba yao na kuelekeza namna ya kuitumia mbolea hiyo. Semina ilifanyika siku ya ijumaa tarehe 29 Aprili 2016 kuanzia saa 5 asubuhi.

Katika semina hiyo, Professor Gao Xiang na Bi Xu Ruijie walifundisha mambo mengi sana. Kwa kifupi walieleza haya kuhusiana na mbolea hiyo inayotengenezwa na kampuni ya Green World.

. Mbolea hiyo yenye ujazo wa lita moja huweza kuchanganywa na lita 1000 za maji kabla ya kutumika. Mbolea hii ambayo hutumika kwa kunyunyizia juu ya majani ya mimea ina uwezo wa kutumiwa kwenye eneo la shamba la ukubwa wa hekta 6.7.

. Kama mkulima atataka kutumia kwenye eneo dogo kama la bustani, atamimina kifuniko kimoja ambacho kina ujazo wa ml 50 na kuchanganya na lita 25 hadi 50 za maji.

. Mbolea hii inaweza kutumika kwa mimea ya aina zote; matunda, nafaka, mboga na hata mimea inayotunza chakula chini ya ardhi kama mihogo, karoti n.k. Mimea iliyonyunyiziwa mbolea haina madhara ikiliwa na binadamu au mifugo – maana yake mbolea hii haina sumu.

. Matumizi mazuri ya mbolea hii ni kuinyunyiza mapema alfajiri au baada ya jua kuzama. Jua kali huharibu amino acids zilizotumika kuitengeneza mbolea hii.
Kuna maelezo mengine mengi yanayomfaa yule apendaye kulima bustani au wakulima wenye mashamba makubwa. Kwa bahati nzuri wataalamu hao bado wapo nchini na wanaendelea na mafunzo kuhusu mbolea hii.

Ratiba yao wakiwa hapa nchini ni kama ifuatavyo.

Tarehe 30/4       Morogoro                                Bright Star Hotel
Tarehe 04/5       Arusha                                       Palson Hotel
Tarehe 02/5      Green World Office DSM
Tarehe 05/5      Green World Office DSM
Tarehe 06/5      Green world Office DSM
Tarhe 07/5        Green world Office DSM
Tarehe 09/5     Green world Office DSM

Wito wangu ni kwa wapenzi wa kilimo kuja kujisikilizia wenywe kuhusu mbolea hii. Kampuni inamkaribisha ye yote anayependa kujua au kuinunua mbolea hii. Hakuna kiingilio kwenye semina hizi na vinywaji vinatolewa. Kupata maelezo zaidi unaweza kuwasiliana nasi 0655 858027 au 0756 181651 au kutuandikia promota927@gmail.com.

 

Usisite kuuliza swali lo lote ulilo nalo au kutoa maoni yako kuhusu mada hii. Ni furaha kwetu kuona kuwa tumekujibu na kwa wakati mwafaka.
Laurian.

 

Pata Mahitaji Yako Ya Dawa Za Nje Kwa Matatizo Yanayokusumbua Ukiwa Tanzania. Boresha Afya Yako Kupitia Tovuti Hii